AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   25th July 2008
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Matukio
 Matukio ya Kale
 Calenda ya Matukio

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Matukio

Matukio

Orodha ya Matukio yajayo:

Mchanganyiko wa kinga
25th Jun 08 ,

Mchanganyiko wa kinga ya Malaria kwa watoto wapatikana
 
Jitihada za watafiti wa tiba sahihi ya ugonjwa wa malaria kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano katika nchi za Afrika Mashariki chini ya ufadhili wa kampuni ya madawa ya Ubeligiji -DAFRA- zimefanikisha kupata dawa maalum ya maji na yenye mchanganyiko wa kinga ya Malaria kwa watoto.

Kwa mujibu wa taarifa za utafiti huo ulifanywa kwa ushirikiano wa wataalam wa mashirika ya utafiti wa malaria kutoka Tanzania, Kenya na Uganda dawa hiyo ni mwendelezo wa juhudi za wadau na mashirika ya kimataifa katika kutokomeza ugonjwa wa malaria unaosababisha vifo vya watu wengi duniani kila mwaka hususani watoto wadogo na wajawazito.


Warsha kubwa ya HMIS kanda ya ziwa
12th Jun 08 ,

Afyamtandao kwa kushirikiana na Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC) pamoja na Taasisi ya Kimataifa ya Mawasiliano na Maendeleo (IICD) inaandaa warsha ya siku moja ya mfumo wa uhifadhi wa taarifa za Afya (HMIS), kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA),warsha ambayo itafanyika Mwanza siku ya Ijumaa tarehe 4/07/2008 katika ukumbi wa Nyakahoja.


Wadau wa Afya kutoka mikoa ya kanda ya ziwa (Mwanza,Mara,Shinyanga na Kagera) watashiriki katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.


Lengo kuu la warsha hiyo ni kwa washiriki kujifunza jinsi mfumo wa uhifadhi wa taarifa za afya kupitia TEKNOHAMA unavyotumika katika hospitali,Changamoto na uwezekano wake.Lakini pia kuboresha na kuongeza ujuzi katika mfumo huo.


Watoto wa ajabu wazaliwa
18th Mar 08 ,

Watoto watatu wa ajabu wamezaliwa huku mmoja akiwa hana kichwa katika Manispaa ya Zanzibar na kuzusha mjadala mzito miongoni mwa wananchi na wataalamu wa afya.

Ofisa Muuguzi wa Wodi ya Wazazi katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja visiwani humu, Bi. Valeria Rashid amesema watoto hao walizaliwa kwa nyakati tofauti wakiwa na maumbile yasiyokuwa ya kawaida.


Amesema mtoto wa kwanza alizaliwa Mwezi Januari, mwaka huu akiwa hana kifua, tumbo likiwa kubwa huku mikono na miguu yake ikiwa mifupi,na mtoto wa pili amezaliwa mwezi Februari, ambaye hakuwa na kichwa huku macho yake yakiwa nje na aliishi kwa muda wa siku tano hospitalini hapo kisha akafa.
 
Mtaalamu huyo ameeleza baadhi ya sababu ya watoto kuzaliwa katika mazingira yasiyokuwa ya kawaida kuwa ni mama mjamzito kuwa na maji mengi katika mfuko wa uzazi.

 


      
Matukio ya Kale
  Hakuna Kitu!.

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007 AfyaMtandao.