12th Jun 08 ,
Afyamtandao kwa kushirikiana na Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC) pamoja na Taasisi ya Kimataifa ya Mawasiliano na Maendeleo (IICD) inaandaa warsha ya siku moja ya mfumo wa uhifadhi wa taarifa za Afya (HMIS), kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA),warsha ambayo itafanyika Mwanza siku ya Ijumaa tarehe 4/07/2008 katika ukumbi wa Nyakahoja.
Wadau wa Afya kutoka mikoa ya kanda ya ziwa (Mwanza,Mara,Shinyanga na Kagera) watashiriki katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Lengo kuu la warsha hiyo ni kwa washiriki kujifunza jinsi mfumo wa uhifadhi wa taarifa za afya kupitia TEKNOHAMA unavyotumika katika hospitali,Changamoto na uwezekano wake.Lakini pia kuboresha na kuongeza ujuzi katika mfumo huo.