AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
Kituo cha Afya Nyakato
Image

 

Kituo cha Afya Nyakato na matumizi ya TEKNOHAMA.

Kukua kwa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) kumeleta mafanikio makubwa katika sekta ya afya nchini Tanzania, ambapo huduma hiyo imeboreka kwa kiwango kikubwa kwa baadhi ya hospitali,vituo vya afya na Zahanati ambazo zinatumia mfumo huo katika kutoa huduma.
 

Kituo cha Afya Nyakato kilichopo jijini Mwanza, ambacho kinamilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Tanzania (KKKT),Dayosisi ya ziwa Victoria,kinatumia teknolojia hii katika kutoa huduma ambapo kimefanikiwa kwa takribani asilimia 80 kuifanya huduma hiyo kuwa bora zaidi na kuleta chachu ya Maendeleo kituoni hapo kwa kutoa huduma ya haraka  kwa watu wanaopata tiba katika kituo hicho.

Dkt.Bonaventura Mazezele Mganga Mfawidhi wa kituo hicho anasema Teknolojia hiyo ya matumizi ya Kompyuta  imeanza kutumika kituoni hapo kuanzia  mwaka 2006 kwa baadhi ya idara kama vile Mapokezi na Ofisi ya  Mganga Mkuu.

Mwaka 2007 ndipo teknolojia hiyo ilipoanza kutumika rasmi baada ya kuanza kutumia “Software” (Programu)ya Afya-pro ambayo imetengezezwa maalumu kwa matumizi ya hospitali  ambayo inahifadhi taarifa za Mgonjwa,Takwimu pamoja na data.
 

Software hii ambayo .imebuniwa na Kampuni ya Teknolojia (NPK) ya jijini Dar es salaam,mbali ya kuwa na uwezo wa kuhifadhi taarifa za Mgonjwa na takwimu, pia ina uwezo wa kuendesha stoo ya madawa ambapo inamwezesha msimamizi wa stoo kujua kirahisi idadi ya dawa zilizopo stoo na zile ambazo zimekaribia kuharibika, inauwezo wa kumpa taarifa mhusika kuwa aina fulani za dawa zimekaribia kuisha hivyo ajiandae kuagiza zingine.

Dkt.Mazezele anasema, hapo mwanzo kabla ya kuanza kutumia mfumo huo utendaji kazi  ulikuwa mgumu, kwani kazi nyingi zilifanyika kwa njia ya mikono,kadi za wagonjwa utunzwaji wake ulikuwa si mzuri na nyingi ziliharibika,wagonjwa walichukua muda mrefu kumuona Daktari kutokana na foleni kubwa iliyokuwepo,usimamizi wa madawa na uandaaji wa ripoti ilikuwa ni tatizo kubwa kwani ripoti zilichukua wiki nzima kuandaliwa, upotevu wa mapato ulikuwa mkubwa, kwa ujumla kazi likuwa ni ngumu.

Daktari anasema baada ya mfumo huo kuanza kutumika kituoni hapo wamepata mafanikio makubwa ambapo kazi za mikono (paper work) zimepungua, kwani mfumo huo kwa sasa  unatoa ripoti haraka na kuzalisha kadi za wagonjwa,unahifadhi taarifa za mgonjwa kirahisi na kutunza data,mapato yameongezeka,idadi kamili ya wagonjwa wanaofikia kituoni hapo kupata tiba inafahamika kirahisi.

Pamoja na mafanikio hayo,Dkt.Mazezele anasema kuna mapungufu machache ambayo bado yanawakabili ili kuifanya huduma hiyo iwe bora zaidi.Ameyataja mapungufu hayo kuwa ni pamoja na upungufu wa kompyuta, kompyuta zilizopo hatoshi,hivyo anaomba mamlaka husika kulifanyia kazi suala hilo.

 

Imewekwa: 27th Nov 08 na Renatus J Sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.