AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
Mafunzo

Mafunzo ya uwezeshaji


Baadhi ya wafanyakazi wa miradi inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Mawasiliano na Maendeleo (IICD) la nchini Uholanzi, wamepewa mafunzo ya uwezeshaji katika  kuboresha shughuli zao.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Nyakahoja jijini Mwanza yalihusisha watumishi wa hospitali katika idara za Mapokezi na Maabara,yalilenga kumjenga muhusika kujitambua, kujiamini na kuwa na uwezo wa kuongoza warsha, semina na kuhudumia watu wa aina mbalimbali.

Katika mafunzo hayo washiriki walifundishwa sifa za kuwa mwezeshaji mzuri ambazo ni pamoja na kuwa na maandalizi ya kutosha kabla ya kufanya kikao au Semina,kufuata utaratibu katika kuongeza semina, kuwa mbunifu katika kazi, kusoma hadhira uliyonayo na kuielewa, kujenga mahusiano na washiriki wengine na kutumia lugha inayoeleweka.

Mafunzo hayo ya siku tano yalihusisha washiriki kutoka Mradi wa kuhifadhi taarifa za afya kwa kutumia Kompyuta (DHMIS), AfyaMtandao na wengine kutoka hospitali za Bukumbi, Kituo cha afya Nyakato ELCT, Zahanati za Makongoro na Nyakahoja.

Kwa upande wao washiriki wameshukuru kwa mafunzo hayo na kuahidi kuwa watatumia ujuzi walioupata kuboresha kazi zao,pia kuwashirikisha wenzao ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika mafunzo.  

 

Imewekwa: 17th Dec 08 na Renatus J Sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.