Mbali na kuanza Januari mwaka jana ikiwa imejikita mikoa ya kanda ya ziwa,mradi huo kwa mwaka huu utapanuka na kufika katika mikoa ya kanda ya kaskazini lakini ukiwa na lengo la kuenea maeneo mengine nchini kurahisisha huduma za utunzaji na upatikanaji wa taarifa za afya.
Hiyo ni pamoja na kuziunganisha hospitali za kanda hizo na miradi midogo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) inayofadhiliwa na Shirika la Mawasiliano na Maendeleo la Uholanzi (IICD).
Afisa Habari wa AfyaMtandao,Renatus Sona amesema baadhi ya hospitali tayari zimejiunga na kuwa wanachama wa AfyaMtandao,amezitaji hospitali hizo kuwa ni Sumve,Bunda,Sengerema,Burongwa,Kolandoto,Kagondo,Rubya na Zahanati ya Ukombozi.