AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
AfyaMtandao

 

Kubadilishana Maarifa Miongoni mwa Wataalamu wa Afya.

Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika utoaji na usimamizi wa huduma za Afya nchini Tanzania bado ni mageni.AfyaMtandao inawaleta pamoja watoa huduma za afya,watungaji wa Sera na wadau wa Maendeleo katika kupanua wigo na kubadilishana maarifa katika maeneo mbalimbali ya Afya.

Maeneo haya yanajumuisha;Tibamtandao (Kutibu wagonjwa kwa kupata maelekezo kutoka kwa madaktari wengine kwa njia ya Mtandao),Usimamizi wa utunzaji taarifa kwa njia ya mtandao (HMIS) na Masomo kwa njia ya Kompyuta au Mtandao (e-learning kwa watumishi wa Afya).AfyaMtandao inafadhiliwa na Taasisi ya kimataifa ya Mawasiliano  ya nchini Uholanzi (IICD) kwa ushirikiano na Shirika la Swiss agency tangu 2006.


Kujenga jukwaa la kushirikishana uzoefu na hospitali zingine.

Mikakati ya kuboresha Mawasiliano katika sekta ya Afya imeenea nchi nzima na kila aina ya hospitali ina mpango wake. Kutokuwa na umoja ikiwa na maana kuwa kutokuwa na sauti za pamoja, makubaliano ya pamoja au majadiliano ambapo mashirika na taasisi zinazotoa huduma ya Afya zinaweza kubadilishana na kujifunza uzoefu ambao watanufaika nao.

AfyaMtandao inajaribu kuziba pengo hilo kwa kujenga jukwaa la majadiliano ambapo wataalamu wa TEKNOHAMA (ICT) katika huduma ya afya wataweza kubadilishana maarifa na kuweka sera kama muongozo katika kazi.Mtandao unasimamia mahitaji kutoka kwa wanachama wake.

 

Imewekwa: 27th Feb 09 na Renatus J Sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.