AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
Makala za Television


Mafanikio ya huduma za afya kwa njia ya makala za Television

Tume ya Kikristo ya huduma za Jamii (CSSC) kupitia mradi wake wa  Afyamtandao, inaendesha  kitengo maalum “Media Unit” cha kutengeza makala na vipindi mbalimbali vya Television vinavyohusu mafanikio ya utoaji huduma za afya, miradi, makongamano, warsha, semina na matukio mbalimbali ya kijamii.

Lengo la kuwa na kitengo hiki ni kuboresha huduma ya afya kupitia makala mbalimbali za TV zenye kuonyesha mafanikio yanayotokana na sekta hiyo.Mfano katika utoaji huduma za afya kuna baadhi ya hospitali ambazo zimefanikiwa kuboresha huduma hizo kwa kiwango kikubwa  hivyo hospitali zingine zitahitajika kujifunza mbinu zilizotumika kuleta mafanikio hayo.  

Kwa kutambua hilo AfyaMtandao imetekeleza kwa kutengeneza makala ambazo zinaovyesha mafanikio katika sekta hiyo na ushirikiano baina ya hospitali za makanisa na serikali.

Makala zilizokwisha kutengenezwa na zingine kuzambazwa kwa wadau.

Makala ambazo kitengo hicho kimetengeneza mpaka sasa ni kuhusu Tibamtandao jinsi inavyofanya kazi kwa baadhi ya hospitali za kanda ya kaskazini, mafanikio ya utoaji huduma za afya mkoani Rukwa ambayo yanayokwenda sambamba na malengo ya milenia, Mfumo wa kuhifadhi na kusimamia taarifa za afya ngazi ya wilaya kupitia “Software” ya AfyaPro katika mkoa wa Mwanza, na njia ya kuwalea watoto ambao hawajatimiza muda wa miezi tisa ya kuzaliwa maarufu kama “Kangaroo method”njia ambayo inatumiwa na hospitali ya teule ya wilaya ya Sengerema.

Nakala kadhaa za makala hayo zimekwisha sambazwa kwa wadau wa afya na wahisani kwa lengo la kushirikishana maarifa na ujuzi huo kutoka katika hospitali   zetu.Wadau wote mnakaribishwa kutumia kitengo hiki ili kutangaza shughuli zenu.

 

Imewekwa: 27th Feb 09 na Renatus J Sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.