AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
Maabara ya kutengeneza ARV

 

Maabara ya kutengeneza ARV yazinduliwa MUHAS


Chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba Muhimbili (MUHAS), kimezindua maabara ya mafunzo ya utafiti na kutengeneza dawa, kwa ajili ya kuboresha mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa famasia kwa malengo ya kutengeneza dawa ili kupunguza uagizaji kutoka nje.

Maabara hiyo ya kisasa itakuwa ikitengeneza dawa za aina mbalimbali kama vile ARV kwa ajili ya kuwaongezea siku wagonjwa wa UKIMWI, Paracetamol kwa ajili ya kutuliza maumivu na vidonge vingine jambo ambalo litasaidia watanzania kupata dawa hizo kwa urahisi.


Mbali na kutengeneza pia maabara hiyo itafanya vipimo kwa dawa zitakazokuwa zinaagizwa ili kujua kama ni bandia au siyo, ili kuwa na uhakika wa dawa zinazotumiwa na wateja wao.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha kimataifa cha German Action Medeor, Bw.Christopher Bonsmann amesema lengo kubwa la kujenga maabara hiyo ni kujaribu kutengeneza mazingira mazuri kwa wanafunzi na walimu wa MUHAS, ili kujifunza kwa vitendo na kuwapa uwezo wa kuzalisha dawa hata watakapohitimu mafunzo yao.

Ujenzi wa maabara hiyo umefadhiliwa na Serikari ya Tanzania kwa asilimia 55, Ujerumani GTZ kwa kushirikiana na Action Medeor asilimia 30, ambapo asilimia 15 zilikamilishwa na MUHAS kwa lengo la  kuongeza ubora wa kutengeneza dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Tanzania imekuwa ikiagiza asilimia 80 ya dawa kutoka nje ya nchi na sasa imejipanga kupunguza uagizaji huo kwa asilimia 50.

 

Imewekwa: 15th Jun 09 na Renatus J Sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.