AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   8th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 
 Habari
 Habari za Kale

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Habari

Habari


Print page  
Mkutano wa tathimini ya miradi ya IICD

 

Matumizi ya Kompyuta yaboresha huduma ya afya Mwanza

Imeelezwa kuwa matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEKNOHAMA) katika sekta ya afya yamechangia kuleta mabadiliko makubwa kwa hospitali, vituo vya afya na zahanati ambazo tayari zimeanza kutumia mfumo mkoani Mwanza.

Washiriki wa mkutano wa tathimini ya miradi ya IICDHayo yamebainishwa na washiriki wa mkutano wa tathimini ya Miradi inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Mawasiliano na Maendeleo (IICD) la nchini Uholanzi.

Meneja mradi wa mfumo wa Kompyuta wa DHMIS unaotekelezwa na baadhi ya hospitali za mkoa wa Mwanza, Bw. Deogratias Kattonyella amesema tangu kuanza kwa utekelezwaji wa mradi huo hospitali za Bukumbi na Nyamagana, Vituo vya afya vya Nyakato na Makongoro na zahanati za Nyakahoja na Nassa zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma ambapo wagonjwa wamekuwa wakipata huduma kwa muda mfupi hali ambayo imechangia wagonjwa wengi kupata huduma ya haraka na isiyokuwa na msongamano.


Aidha Bw. Kattonyella amedai kuwa mfumo huo umechangia hospitali kuwa na ripoti sahihi kutokana na takwimu kuhifadhiwa katika Kompyuta.

Kwa upande wake Bi. Pauline Kimollo ambaye anasimamia mradi wa Kompyuta unaotumia mfumo wa Care2x amesema, matumizi hayo ya Kompyuta yameweza kusaidia hospitali nyingi kujua idadi ya mapato yanayokusanywa kwa siku sambamba na idadi za dawa zilizopo Stoo hivyo hakuna aina yeyote ya udanganyifu unaojitokeza katika mfumo huo.  

Akizungumza katika mkutano huo mwakilishi kutoka ofisi ya mganga wa jiji Dk.Kokugonza Mugeye amesema kuwa baada ya mafanikio ya kutumia mfumo wa Kompyuta kuonekana katika hospitali ya Wilaya ya Nyamagana, Halmashauri ya jiji la Mwanza inategemea kuviunganisha vituo vingine 8 vya Serikali katika mfumo huo mwaka huu.

Pamoja na mafanikio hayo kupatikana, ni changamoto chache zimejitokeza katika mfumo huo ambazo ni pamoja na; tatizo la umeme kwa baadhi ya vituo vya afya, vifaa vya mfumo (Kompyuta) na kukosekana kwa mafunzo ya kutosha kwa watumishi.Miradi hiyo  inayofadhiliwa na IICD ni; AfyaMtandao, DHMS (AfyaPro), HMIS (Care2x), Telemedicine, TEKNOHAMA hospitali ya wilaya ya Magu na Sengerema, e-learning.   


 

Imewekwa: 6th Jan 10 na Renatus sona

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.