AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   25th July 2008
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Miradi ya Afya

Miradi ya Afya

Muhtasari
Uwezo wa kukusanya, kuchambua na kutumia taarifa sahihi ni muhimu katika kuwawezesha wafanyakazi wa sekta ya afya kutoa huduma  bora kwa ufanisi.Aidha kupatikana kwa taarifa sahihi na kwa wakati ni muhimu katika kuwawezesha  waandaaji wa sera  kufanya maamuzi sahihi.

Cha kusikitisha ,hali ya sasa sivyo ilivyo.Taarifa zinazokusanywa kwa kutumia karatasi na kalamu  zinakabiliwa na upotoshaji, upotevu na uharibifu na zinachukua muda mrefu kuwekwa katika mfumo wa matumizi,hatua nyingine inayohatarisha usahihi  wake. Ubora  wa huduma za fya zitolewazo unaathiriwa vibaya na  matatizo ya mawasiliano na uhaba wa vyazo vya habarí za   afya na tiba kama vile majarida. Taasisi za afya za AICT zinakabiliwa na matatizo makubwa ya kupata  kwa wakati taarifa sahihi na ni mara chache  waandaaji sera wanapata  taarifa muhimu za kuwasaidia katika kufanya maamuzi.

Uanzishwaji wa Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji Huduma za Afya Wilayani una lengo la kutumia Teknohama(ICT) kuimarisha  uwezo wa kukusanya, kuchambua na kuhifadhi taarifa za afya  katika ngazi ya wilaya  kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya, kuhakikisha usahihi wa taarifa na hatua zinazochukuliwa  pamoja na kuongeza uwajibikaji na kutoa picha sahihi ya mienendo ya afya wilayani.

Hali ilivyo sasa
Mradi huu ulianza Februari 2006 na unaendelea.Mapitio ya kwanza ya mradi yalifanyika mwishoni mwa Septemba 2006


Muhtasari
Kinondoni ilikuwa ya mwanzo kuanzisha  MTUHA katika ngazi ya Manisipaa Mradi huu unalenga kuimarisha  zaidi mipango ya afya na matumizi ya Teknohama(ICT) katika taasisi za afya


Muhtasari
Uendeshaji wa taasisi za afya unakabiliwa na  tatizo la uongozi dhaifu kutokana na uhaba wa watendaji , kuondoka kwa wataalamu  na matumizi hafifu ya taarifa. Taarifa zinazopatikana kutoka kwenye taasisi za afya hazina ubora  na zinawachukua watendaji muda mrefu kuziandaa.Miundombinu ya Teknohama(ICT) iliyoko Tanzania hivi sasa inawezesha baadhi ya taasisi za afya kutumia mtandao wa kompyuta  kuandaa taarifa  za uendeshaji huduma za afya .
Mradi huu unalenga kuandaa mifumo mahsusi ya uendeshaji  huduma za afya kwa ajili ya taasisi za KKKT Mifumo hiyo ya MTUHA itakuwa hususan kwa ajili ya taasisi hizo lakini pia itakuwa  inakidhi viwango na mahitaji ya MTUHA ngazi ya Taifa.

Muhtasari

Afyanet Tanzania imekusudiwa kuwa mtandao unganishi kwa ajili ya sekta ya afya.Utatoa huduma bora kwa wateja na  kuziunganisha taasisi za afya kwenye mtandao. Kwa mfano,sekta ya afya Tanzania ina miradi mingi kama vile ile ya malaria na Ukimwi.Kwa sababu kila mradi unajitegemea uratibu katika sekta ya afya unakuwa mgumu kwa sababu ya kukosa ushirikiano na mawasiliano.Kukiwepo na kiungo kimoja cha miradi yote ya sekta ya afya miaradi hii itashirikiana na kuboresha huduma kwa wateja.

CSSC inasimamia karibu asilimia 40 ya sekta ya afya hapa nchini.Kuanzishwa kwa Intranet katika CSSC kutasaidia  kupanua matumizi ya teknohama(ICT) katika kuimarisha mawasiliano na upeanaji maarifa na  taarifa. Kuwapatia elimu viongozi wa makanisa kuhusu teknohama kutasaidia kuharakisha mchakato wa kuanzishwa kwa Afyanet Tanzania na kukubalika kwake.


Muhtasari

Gharama za kujiunga katika tovuti bado ziko juu sana hapa Tanzania.Lakini kwa kuungana na kushirikiana katika  kununua bandwidth gharama hizo zinaweza kupungua kwa karibú asilimia 40. Taasisi nyingi za afya bado zinakabiliwa na ukata na hazina vyazo vya uhakika vya mapato licha ya kwamba nyingi ya hizo bado hazijaweza hata kujiunga katika mtandao au hata kuanzisha matumizi ya kompyuta katika ofisi zake.
Lengo  lingine la kuanzishwa kwa mradi huu wa Afyanet  ni kwamba iwe  chombo kitakachounganisha taasisi za afya katika  mazungumzo ya kibiashara ya ununuzi wa bandwidth kwa ajili ya kuuunganisha taasisi hizo kwenye tovuti. Aidha Afyanet itatoa pia huduma za kiufundi kwa wanachama wake na wateja wengine kwa jumla.


Muhtasari

Gharama za kujiunga katika tovuti bado ziko juu sana hapa Tanzania.Lakini kwa kuungana na kushirikiana katika  kununua bandwidth gharama hizo zinaweza kupungua kwa karibú asilimia 40. Taasisi nyingi za afya bado zinakabiliwa na ukata na hazina vyazo vya uhakika vya mapato licha ya kwamba nyingi ya hizo bado hazijaweza hata kujiunga katika mtandao au hata kuanzisha matumizi ya kompyuta katika ofisi zake.
Lengo  lingine la kuanzishwa kwa mradi huu wa Afyanet  ni kwamba iwe  chombo kitakachounganisha taasisi za afya katika  mazungumzo ya kibiashara ya ununuzi wa bandwidth kwa ajili ya kuuunganisha taasisi hizo kwenye tovuti. Aidha Afyanet itatoa pia huduma za kiufundi kwa wanachama wake na wateja wengine kwa jumla.


P3-30.310: HIV/AIDS Uelimishaji na ubadilishaji tabia za Vijana

VVU/UKIMWI (HIV/AIDS) ni janga la kimataifa. Vijana wengi hasa wa vijijini bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu janga hili. CSSC ambacho ni chombo cha  makanisa  yenye waumini ambao ni sehemu kubwa ya jamii bado haina  taarifa na mikakati inayokubalika kwa wadau wake ya kukabiliana na janga hili Teknohama(ICT) ni njia mojawapo  ya kuwezesha uandaaji na usambazaji wa taarifa kuhusu namna ya kupambana na ukimwi. Katika mradi huu, vikundi vya wanafunzi vikisaidiwa na wataalamu vinaandaa mikakati ya kuelimishana  kwa vijana wa rika mbalimbali pamoja na wazazi wao na waumini wengine kwa jumla. Vielelezo na maigizo ni moja ya njia zinazotumika kutoa elimu hii


P3-30.310: HIV/AIDS Uelimishaji na ubadilishaji tabia za Vijana

VVU/UKIMWI (HIV/AIDS) ni janga la kimataifa. Vijana wengi hasa wa vijijini bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu janga hili. CSSC ambacho ni chombo cha  makanisa  yenye waumini ambao ni sehemu kubwa ya jamii bado haina  taarifa na mikakati inayokubalika kwa wadau wake ya kukabiliana na janga hili Teknohama(ICT) ni njia mojawapo  ya kuwezesha uandaaji na usambazaji wa taarifa kuhusu namna ya kupambana na ukimwi. Katika mradi huu, vikundi vya wanafunzi vikisaidiwa na wataalamu vinaandaa mikakati ya kuelimishana  kwa vijana wa rika mbalimbali pamoja na wazazi wao na waumini wengine kwa jumla. Vielelezo na maigizo ni moja ya njia zinazotumika kutoa elimu hii


Muhtasari
KJatika baadhi ya maeneo vijijini,ukeketaji wanawake  bado  ni mila  inayoendelezwa na kuchukuliwa kama kinga dhidi ya magonjwa kama m alaria, homa ya mapafu na ukimwi.Kuwaelimisha wananchi na waganga wa jadi ni njia mojawapo ya kukabiliana na tatizo hili. Tanzania Inter African Committeé (TIAC) inatambua kwamba ingawa dunia imejaa bado  elimu ya  kutosha ya afya  haijafika vijijini. Mradi huu una lengo la kusambaza elimu ya afya vijijini ili kukabiliana na mila potofu zinazodhuru afya za wananchi kama ile ya ukeketaji wanawake.

PROGRAMME 4: MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA KAZINI
CONTINUING PROFESSIONAL DEVELOPMENT(CPD)
PROGRAMME 4: MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA KAZINI
CONTINUING PROFESSIONAL DEVELOPMENT(CPD)
Elimu kuhusu Afya ya Uzazi

P4-30.322:CPD-MAFUNZO ENDELEVU KWA MEDICAL CLINICIANS

Taasisi Kiongozi: KCMC


P5-30.310:ICT4 UCHUNGUZI NA TIBA
Muhtasari
Mradi huu pia una lengo la kutoa huduma ya uchunguzi wa kidaktari na tiba kwa njia ya mtandao wa kompyuta nchini Tanzania

Muhtasari
Mradi huu pia una lengo la kutoa huduma ya uchunguzi wa kidaktari na tiba kwa njia ya mtandao wa kompyuta nchini Tanzania

P6-30.315: SERA YA TEKNOHAMA NA MKAKATI WA UTEKELEZAJI WAKE


P6-30.316:MKAKATI WA TEKNOHAMA KWA WANACHAMA WA CSSC


 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007 AfyaMtandao.