P3-30.310: HIV/AIDS Uelimishaji na ubadilishaji tabia za Vijana VVU/UKIMWI (HIV/AIDS) ni janga la kimataifa. Vijana wengi hasa wa vijijini bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu janga hili. CSSC ambacho ni chombo cha makanisa yenye waumini ambao ni sehemu kubwa ya jamii bado haina taarifa na mikakati inayokubalika kwa wadau wake ya kukabiliana na janga hili Teknohama(ICT) ni njia mojawapo ya kuwezesha uandaaji na usambazaji wa taarifa kuhusu namna ya kupambana na ukimwi. Katika mradi huu, vikundi vya wanafunzi vikisaidiwa na wataalamu vinaandaa mikakati ya kuelimishana kwa vijana wa rika mbalimbali pamoja na wazazi wao na waumini wengine kwa jumla. Vielelezo na maigizo ni moja ya njia zinazotumika kutoa elimu hii
|