AfyaMtandao | Msaada | Wasiliana nasi | Maoni | English Version
Tafuta :    
 Mwanzo  | Kuhusu AfyaMtandao  | Habari  | Matukio  | Huduma za Afya  | Maswali Mrudio(FAQ)  | Afya Akaunti  | Links   9th September 2010
                                 
    Magonjwa, jinsi ya kuzuia na kujikinga   Makala za Afya kutoka kwa wataalamu wa afya   Maswali na majibu kuhusu masuala ya afya   Afya Yako na jinsi ya kuiboresha   Afya Katika Picha na maelezo  
                                 
 

 

 
      
Mahali Ulipo:  » Mwanzo » Miradi ya Afya

Miradi ya Afya

Maelezo zaidi
Malezo ya Mradi

Muhtasari
Uwezo wa kukusanya, kuchambua na kutumia taarifa sahihi ni muhimu katika kuwawezesha wafanyakazi wa sekta ya afya kutoa huduma  bora kwa ufanisi.Aidha kupatikana kwa taarifa sahihi na kwa wakati ni muhimu katika kuwawezesha  waandaaji wa sera  kufanya maamuzi sahihi.

Cha kusikitisha ,hali ya sasa sivyo ilivyo.Taarifa zinazokusanywa kwa kutumia karatasi na kalamu  zinakabiliwa na upotoshaji, upotevu na uharibifu na zinachukua muda mrefu kuwekwa katika mfumo wa matumizi,hatua nyingine inayohatarisha usahihi  wake. Ubora  wa huduma za fya zitolewazo unaathiriwa vibaya na  matatizo ya mawasiliano na uhaba wa vyazo vya habarí za   afya na tiba kama vile majarida. Taasisi za afya za AICT zinakabiliwa na matatizo makubwa ya kupata  kwa wakati taarifa sahihi na ni mara chache  waandaaji sera wanapata  taarifa muhimu za kuwasaidia katika kufanya maamuzi.

Uanzishwaji wa Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji Huduma za Afya Wilayani una lengo la kutumia Teknohama(ICT) kuimarisha  uwezo wa kukusanya, kuchambua na kuhifadhi taarifa za afya  katika ngazi ya wilaya  kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya, kuhakikisha usahihi wa taarifa na hatua zinazochukuliwa  pamoja na kuongeza uwajibikaji na kutoa picha sahihi ya mienendo ya afya wilayani.

Hali ilivyo sasa
Mradi huu ulianza Februari 2006 na unaendelea.Mapitio ya kwanza ya mradi yalifanyika mwishoni mwa Septemba 2006

Historia ya mradi Mradi huu ulianza Februari 2006 na unaendelea.Mapitio ya kwanza ya mradi yalifanyika mwishoni mwa Septemba 2006
Goal

Maendeleo
Utekelezaji wa MTUHA utahakikisha kuwa taarifa sahihi zinapatikana kwa wakati.Hatua hiyo itahakikisha utoaji bora wa huduma za afya na maamuzi sahihi kuhusu sera

Objectives Malengo
Lengo kuu la mradi  ni kutumia ICT katika MTUHA ili kumwezesha Daktari wa Jiji la Mwanza (CMO), The Africa Inland Church Tanzania (AICT), Kanisa la Kikristo la Kilutheri Tanzania(KKKT) na Kanisa Katoliki(RC) na wabia wao katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza katika  kutumia tekinolojia hii ya kisasa kuendesha shughuli za afya kwa ufanisi na  kutoa huduma bora kwa wananchi.
Malengo mahsusi ya kuwezesha  mradi wa MTUHA kufikia lengo lake kuu ni:-
• Utekelezaji wa MTUHA katika ngazi ya wilaya
• Mafunzo kwa watumuaji wa MTUHA
• Kuwafungua macho wadau wengine na watumishi wa serikali kuhusu MTUHA
• Kujenga uwezo wa kuendesha mradi huo katika makao makuu yake
• Kuunganisha  kwenye  mtandao  taasisi za za AICT, KKKT, RC na CMO
• Kuhakikisha upeanaji taarifa na utendaji bora
Target Utekelezaji wa MTUHA katika ngazi ya wilaya
Mategemeo Soko
Taasisi za Makanisa zitanufaika moja kwa moja kwani mradi wa  MTUHA utasaidia shughuli za kila siku.Wateja watanufaika kwa kupata huduma bora zenye ufanisi. Waandaaji sera watakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya maamuzi yao kwa usahihi na ufanisi na hivyo kulinufaisha taifa kwa jumla
Mafaniko Uendeshaji
Katika mradi huu, AICT ndiyo asasi kiongozi KKKT, RC na CMO wakiwa wabia. Hati ya Makubaliano inayoainisha majukumu ya kila upande imeandaliwa na kukubaliwa.
Mfadhili Fedha
IICD ndiyo mfadhili mkuu wa mradi huu
Barua pepe ridahern@yahoo.com
Mradi Unaanza 0000-00-00
Mradi Unaisha 0000-00-00
Anwani ya Jumla Africa Inland Church Tanzania P.O. Box 905,Mwanza
Simu ya Mezani 0754 442379 / +255(0)28 2500302
Hali ya Mradi
Anwani binafsi Dk.Richard Mbwambo
Anwani ya shirika Africa Inland Church Tanzania P.O. Box 905,Mwanza
Mratibu Dk.Richard Mbwambo
Gharama N/A
Nyaraka : Chukua waraka


« 

 

 

   
 
Haki zote zimehifadhiwa ©2007-2010 AfyaMtandao.