Muhtasari Uendeshaji wa taasisi za afya unakabiliwa na tatizo la uongozi dhaifu kutokana na uhaba wa watendaji , kuondoka kwa wataalamu na matumizi hafifu ya taarifa. Taarifa zinazopatikana kutoka kwenye taasisi za afya hazina ubora na zinawachukua watendaji muda mrefu kuziandaa.Miundombinu ya Teknohama(ICT) iliyoko Tanzania hivi sasa inawezesha baadhi ya taasisi za afya kutumia mtandao wa kompyuta kuandaa taarifa za uendeshaji huduma za afya . Mradi huu unalenga kuandaa mifumo mahsusi ya uendeshaji huduma za afya kwa ajili ya taasisi za KKKT Mifumo hiyo ya MTUHA itakuwa hususan kwa ajili ya taasisi hizo lakini pia itakuwa inakidhi viwango na mahitaji ya MTUHA ngazi ya Taifa.
Historia ya mradi
Wabia:CSSC Wamiliki wa Mradi: KKKT
Goal
Maendeleo MTUHA utaleta mtiririko mzuri wa taarifa zilizoandaliwa kwa usahihi na kupatikana kwa wakati.Hali hii itawezesha uandaaji wa mipango ya afya kwa uhakika zaidi na uchunguzi wa wagonjwa kufanyika kwa makini na haraka zaidi na kwa hiyo wagonjwa wengi zaidi kuhudumiwa.
Objectives
Malengo Malengo ya mradi ni haya yafuatayo:- 1. Kutengeneza programu mahsusi za kompyuta kwa ajili ya taasisi husika lakini pia kukidhi mahitaji ya MTUHA-taifa 2. Kuweka kompyuta katika taasisi husika ili kuwezesha MTUHA kufanya kazi 3. Kuwa na watendaji waliofunzwa namna ya kutumia MTUHA kwa ufanisi 4. Kuhakikisha kunakuwepo huduma za kiufundi caribú na taasisi. 5. Kuhakikisha kuwa kunakuwa na mawasiliano kati ya waendeshaji wa mfumo huo na watumiaji ili kuhakikisha kuwa mahitaji ya watumiaji yanazingatiwa na mfumo unaboreshwa kila mahitaji ya kufanya hivyo yanapojitokeza 6. Kuhakikisha kuwa taasisi zote 26 za afya zinahusishwa katika mfumo huo na mwongozo wa namna ya kutumia mfumo huo na huduma za kiufundi na mafunzo kuhusu tekinolojia hii ya kisasa yanapatikana
Target
Soko Wadau wakuu wa mradi huu ni taasisi za afya za KKKT. Ni kwa manufaa ya watoaji huduma za afya kuwa na mfumo makini wa kukusanya taarifa muhimu za uendeshaji huduma za afya. Ndani ya mfumo huo programu ya MEMS itanufaika sana na mradi huu kwani unawezesha matumizi ya kompyuta katika kuhakiki mali na usimamizi wake. Ndani ya CSSC, taasisi za afya zamakanisa mengine zinafuatilia kwa karibú kuona mafanikio ya mradi huu Wizara ya Afya na Mamlaka za Afya za Mikoa na Wilaya zitanufaika na mradi huu kwani zitapata taarifa bora zaidi ambazo zitakuwa msingi wa kuanzisha matumizi ya kompyuta katika uendeshaji wa huduma za afya. Mradi huu utapunguza mianya ya rushwa na ubadhilifu.Waliokuwa wakinufaika na uovu huo watajaribu kuuhujumu mradi huu. Kwa hiyo utaratibu wa kutoa motisha na mafunzo ya mabadiliko ya fikra kwa waathirika ni mambo yanayohitajika. Wabia wa mradi huu wa Managed Health Care Programme(MHCP) watapenda kuuuona unafanikiwa.
Mategemeo
Uendeshaji Huu utakuwa moja ya miradi iliyoko chini ya Idara ya Afya ya KKKT Timu ya Uendeshaji wa Mradi ndiyo itakayofanya maaamuzi yote muhimu na Meneja wa Mradi ndiye atakayehusika na uendeshaji wa siku kwa siku. Matatizo yatakayojitokeza yatapelekwa kwa Mkurugenzi wa Huduma za Afya wa KKKT
Mafaniko
Hali Halisi ilivyo sasa Mradi umeanza.Mafunzo na maandalizi ya programu za kuendeshea mifumo hiyo inaendelea Warsha kuhusu mabadiliko ya uendeshaji na utendaji kazi ilifanyika Septemba 19-20 2006.
Mfadhili
IICD of the Netherlands
Fedha Wafadhili wa mradi huu ni IICD, Cordaid na MHCP